Historia ya Sheikh Salim Mti Mkavu











Utangulizi

Namshukuru Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa kunijaalia fikra na utashi wa kuandika kitabu hiki nilichokitambulisha kwa jina la سيرة ملهمة (siiratun mulhimah) .Makusudio yangu makubwa katika kuandika kitabu hiki ni kuelezea sifa na mwenendo wa maisha ya Bwana na walii aliye kipenzi cha Mwenyezi Mungu Mtukufu na Mtume (SAW).

Ni Matarajio yetu Historia hii tuliyoiandika ndani ya kitabu hiki itahifadhika na kujenga kumbukumbu juu ya maisha ya watu wema kwa ujumla. Kuwakumbuka watu wema na kufuatisha matendo mema ni ufunguo wa kheri hapa duniani na Akhera.

Insha Allah Mwenyezi Mungu amjaalie kila la kheri msomaji wa kitabu hiki na amjaalie kuwa na matendo mema.
Eee Mwenyezi Mungu tujaalie sote
mwishilio mwema na utujaalie kuwa
watu wa peponi
(Aamiin).
Ustadh Musa Abdulrahman Msele  
+255 717 408 584

              











Sura ya kwanza:
Asili Yake

Bismillaah Rrahmaan Rrahiim



       Ninayekusudia kumhadithia historia yake ndani ya kijitabu hiki jina lake halisi ni Sheikh Salim Ibn Mubaarak Ibn Salim Al- Gahlan. Asili yake ni mwarabu wa asili ya Hazramuut nchini Yemen anayetokana na uzazi wa Sheikh Mubaarak Ibn Salim Al-Gahlan na mama yake Bibi Fatimah. Sheikh Salim amezaliwa nchini Kenya katika mji wa Mombasa kitongoji cha Bondeni mnamo mwezi February  mwaka 1922. Kama ilivyokuwa mash huri na kawaida kwa waja wema wa Mwenyezi Mungu maisha yao hukumbwa na hali na matukio tofauti tofauti ambayo huwa ni bishara na alama za utukufu wao katika maisha yao ya kidini.

 


Sheikh Salim Mubarak Salim Gahlan

Vivyo hivyo Sheikh Salim amepitia katika joto hilo, ikiwa ni ishara kwa wenye akili kutambua utukufu wa darja ya bwana huyu mbele ya viumbe vya Allah.









Sura ya pili
Malezi yake

 





     Bishara hii ilianza kuonekana pale wazazi wake wote wawili kufariki angali mdogo sana na kupelekea kulelewa na babu yake Sheikh Salim Gah Lan na bibi yake upande wa mama yake Bi Sahale binti Khamisi aliyekuwa akiishi kijiji cha Sarigoi Mjini Mombasa.
Hata hivyo babu yake hakumlea muda mrefu akafariki akimuacha Sheikh Saalim chini ya mikono ya bibi yake kwa mama yake Bi Sahale akiwa bado mdogo sana. Hata hivyo bibi yake huyo ( yaani Bi Sahale Binti Khamisi) naye hakikupita kipindi kirefu naye akafariki( hiyo ilikuwa mwaka 1948) akimmwacha sheikh angali mdogo kiumri.
Kutokana na kifo cha bibi yake, nafasi ya malezi yake ilishikwa na mjomba wake bwana Mansuri Bin Abdallah. Vivyo hivyo mjomba wake  haikupita muda mrefu naye akafariki baada ya kumlea masiku machache.
Baada ya kifo cha mjomba wake Mansuri, suala la malezi yake lilikuwa ni swali lililogonga vichwa vya wanandugu hata asijue hata mmoja vipi itakuwa malezi yake baada ya kifo cha mjomba wake. Hapo ndipo Mwenyezi Mungu alipodhihirisha yale yaliyofichikana katika masaibu na mikasa mbalimbali iliyomkumba Sheikh Salim katika makuzi yake.
Lakini kwa rehma na muongozo wa Allah, Sheikh Sharifu Al Habib Swaleh Izzadin ( radhwia llah anhu) alimchukua Sheikh Salim kwa ajili ya kumlea. Wal hamdulillah hapo ndipo ilipopatikana nafasi kubwa kwa Sheikh Salim kujifunza mambo mbalimbali yausuyo dini ya uislam na twariqa kwa ujumla

Sura ya Tatu
Elimu na masheikh zake

 




     Sheikh Salim Mubarak alipata bahati ya kuwa katika kizazi cha wajuzi wa dini. Hii ni kumaanisha kuwa baba yake mzazi Sheikh Mubarak Bin Salim alikuwa ni miongoni mwa wanazuoni jambo lilimsaidia Sheikh Salim kujiegemeza katika kujifunza dini yake tokea utotoni mwake.
   Na hii huwa ni kawaida kwa wenye akili kuwa malezi na mafundisho mema kwa mtoto huanza kwa wazazi wake. Baada ya kuishi muda mdogo na wazazi wake sheikh salim alichukuliwa na babu yake aliyekuwa rafiki wa karibu wa Sheikh Swaleh Izzadin.
Vile vile naye babu yake Sheikh Salim Gahlan naye alikuwa ni miongoni mwa wanazuoni wa kiislam waliokuwa wakiheshimiwa katika zama zake. Hivyo pia Sheikh Saalim alipata nafasi ya kujifunza mas ala kwa babu yake. Baada ya kuondokewa na babu yake na baadae mjomba wake, Sheikh Salim alichukuliwa na Sharifu, Alhabib Sheikh Swaleh Izzadin ambaye ndiye mwalimu wake mkubwa aliyepata  kutoka kwake elimu ya dini yake.
Hapo ndipo ndipo malezi ya Sheikh Salim yakawa yamelenga zaidi tassawf kwa mafunzo ya kiroho, kimwili, na uchamungu kutoka kwa Al Habib Sharif Swaleh Izzadin Al Jailaniy. Hata hivyo elimu yake ilitoka kwa wanazuoni wengi zaidi ya hapa kwani baadae alipitia katika mikono salama yenye kuijua dini mpaka kufikia hadhi ya kuwa  khalifa na sheikh.
Miongoni mwa masheikh zake Alhabib Salim Mti Mkavu ni:-
1.Al Habib Sheikh Sharif Swaleh Izzadin
2. Sheikh Salim Gah lan
3. Sheikh Mubarak Bin Salim ( Baba Yake)
4. Al Habib Sheikh Sharif Muh Dhari
5. Al Habib Sheikh Omari Bin Alli Kullatein
6. Sheikh Sufi  Bin Kabole











Sura ya Nne
Kuanzishwa kwa Madrasa ya Izzadin

 




  Kama alivyochukuliwa sayyid Sheikh Abdul Qaadir Jai Laany na Nabii Khidri kumpeleka Baghdad kwa ajili ya kupata elimu vivyo hivyo ndivyo alivyo fanya Sheikh Sharif Swaleh Izzadin kwa Sheikh Saalim. Baada ya kulitekeleza jambo hilo Sheikh Izzadin alimtoa Sheikh Salim katika mji wa Mombasa kumpeleka hadi Moshi  nchini Tanzania kabla ya uhuru.
Baada ya kumtoa sheikh salim katika mji aliozaliwa mombasa  alimpeleka katika mji wa moshi na akapafanya hapo ndio makazi ya sheikh salim. Baadaye sharifu swalehe akahama katika mji wa moshi akamuusia sheikh saalim kubaki hjapo katika zawiya ya moshi mjini.
Kilipita kipindi kirefu tangu sharifu swlalehe ahame moshi na kumuacha sheykh salim zawiyani.kwa vile sheykh salim alikua na mapenzi makubwa sheykh wake sharifu swaleh basi ikambidi amuombe idhini ili amfuate akaishi naye tena kwani alifurahi kuwa naye karibu zaidi na zaidi.
Alipomfikishia ombi la kutaka kumfuaata,sharifu swalehe akamwambia'kaa Hapo Hapo Moshi Na Ufungue Madrassa Ya Kusomesha Watoto Na Darsa Utakalolifungua Uliite Madrasat-Izzadin' alipopata jibu hili sheykh salim hakusononeka bali alitia bidii juu ya amri aliyopewa na mara moja akafungua darsa katika zawiya ya pasua hapo hapo mjini moshi.
Akaendelea kudar-sisha hapo zawiyani pasua kwa muda kiasi,ndipo alipoombwa na shaushi khamisi lelo wa njoro hapo hapo moshi ahame kutoka alipokua akiishi zawiyani pasua na ahamie njoro.









Chuo cha Izzadini tawi no 2










Shaushi khamisi lelo alimuahidi sheykh salim kua atamuandalia pahala pake pa kukaa katika katika nyumba yake,pia atatoa nafasi kwa ajili ya madrassa.
Sheikh salim alipoombwa hivi hakukataa bali alihama katka zawiya ya pasua na akahamia njoro kwa shaushi khamisi lelo na akafungua dar-sa akawa anasomesha dini.
Mpaka anapokea amri kuanza kusomesha wanafunzi,sheikh salim alikua amepata elimu kwa namna kadhaa,kama vile mafundisho ya ana kwa ana na sharifu swaleh au akasomeshwa kwa ishara.pia alipambanukiwa na jambo lolote liwe la kidunia au dini  kwa namna alivyoitaka mwenyezi mungu mwenyewe. Na bila shaka huo ndio utaratibu waupatao mawalii wa mwenyezimungu.je haijakupambanukia tu kujua kuwa bwana huyu dar-ja yake iko vipi?
Akiwa amefungua dar-sa na anafundisha wanafunzi wake hapo njoro dar-sa yake ilipanuka ikatokea kuwa miongoni mwa dar-sa.na  kwa kipindi chote hicho hakuwahi kutembelewa na mlezi wake waroho sharifu swalehe.
Basi ilipotimia wakati,sharifu swalehe akaja moshi. Kuja kwwake moshi haikuwa bure ila alikuja kwa amri ya mwenyezi mungu. Kwa vile yeye sheikh swaleh ndiye aliyemgundua sheikh salim kuwa ni mwenye darja katika dini, basi mwenyezi mungu akamuamrisha sharifu swaleh aende moshi akambashirie sheikh salim ajijue yeye ni mtu wa cheo gani mbele ya waumini. Sheikh salim akiwa darasani kwake njoro akiendelea kusomesha alipata khabari kuwa sharif swaleh amekuja.





Sura ya Tano
Kifo cha Sharifu Swaleh Izzadin (r.a)
 




     Hapoapo bila simile akatoka hima darasani kwake na akamuwahi sharifu swaleh zawiyani alipoifikia. Sheikh salim alipomtokezea sharif swaleh machoni pake, hapo sharif swaleh akatabasamu na akaita, kumuita sheikh salim akasema" yaa salim bahati yako kubwa" na hapo sharifu swaleh akiwa na hali ya kuumwa akatia fatha nma akaomba dua kwa muda mrefu sana il hali kamuelekea sheikh salim kisha akamruhusu atoke nje. Siku ya pili yake sharif swaleh akafdariki dunia, huo ukiwa ni mwaka 1968. Ulikuwa ni msiba mzito sio kwa sheikh salim tu bali kwa muridi na waislam wote wananomfahamu na wasiomfahamu sharif swaleh.


Ulizima moyo wa sheikh salim mzizimo wote wa huzuni huku akifarijiwa na sharif muhdhar bin hussein al ahdaly ambaye pia ni mpenzi na ndugu kisha khalifa wa sharifu swaleh akamnasihi akamwambia huzunika kwa msiba wa kuondokewa na sharif swaleh, lakini liwazika na radhi alizokupa sharif swaleh na wala hata twezeka hapo dunianio. Maliwazo hayo yalitoka moyoni mwa sharifu muhdhari kumliwaza sheikh salim. Haikutoshea kwa sharifu muhdhari kumliwaza sheikh salim kwa maneno hayo tu balio naye akamfanya kama mwanae na akawanadia wanae wasimtenge sheikh salim kwa jambo lolote litakalofanywa katika familia ya sharifu muhdhari bin husein al ahdany
Anahadithia mwenyewe sheikh salim kuwa tangu alipo husia sharifu muhdhari kwa wanawe hapajakengeukwa kwa hata kidogo mpaka sasa. Baada kuisha kupita huzuni hiyo sheikh salim akaendelea kudarsisha kwa bidii zaisdi ahata wakati mmoja akawafikia mgeni kutoka zanbzibar. Huyo alikuwa sharifu omar bin alliy kulltayn. Lengo la safari ya sheikh omari bin ally toka zanzibar na kuja moshi ni kumzuru sharifu swaaleh izzadin. Basi sharifu omary bin ally kullatayn akifuatana na sheikh salim na jamaa wengine wakaenda hadi kwenye kaburi la sharif swaleh kumzuru.
 Baada kuisha kumzuru sharif swaaleh wakarudi na wakaenda moja kwa moja nyumbani kwa sharif muhdhar. Walipofika nyumbani kwa sharifu muhdhari wakatmkuta sharifu muhdhari yupo mlangoni pake anawasubiri. Walipofika nyumbani aliposimama sharifu muhdhari akaita kwa sauti kubwa." yaa salim nilikuwa na sharif swaleh hapa na maeniagiza ni kwambie kuwa wewe ni khalifa na tena ni sheikh na tena uko juu juu juu" kisha sharifu muhdhari akatia fat ha na akaomba dua hal;afu akawaeleza waliohudhuria kuwa tangu sasa salimu ni khalifa na ni sheikh hivi ndivyo sheikh salim alivyopata ukahalifa na usheikh pia.
 Cheo alichonacho hakupewa kwa utashi wa mtu bali mwenyezi mungu aliridhia malezi aliyopata kwa mabwana wakubwa hawa na akawaridhia muda ukufika wamkabidhi cheo chake. Baada ya hayo kutendeka, haukupita muda mrefu haukupita muda mrefu sheikh muhdhar naye akafariki. Hii inaonyesha jinsi ambavyo kila aliyemlea sheikh salim alikuwa na kazi alizopangia na mwenyezi mungu kuzifanya na kakisha timiza aliloagizwa basi huwa hana buni ila kumuachia mwingine.
Tizama wazazi wake walipo mzaa sheikh saalim jukumu lao likawa liometimia. Ulezi wa awali ukawansibikia babu na bibi yake. Nao kiasi cha ulezi wao kwa sheikh salim kilipotimia fursa ya malezi ikatawaliwa na mjomba wake. Naye jambo lake lilipotimia kwa malezi ya kawaida ndipo malezi ya kiroho yakawa mikononi mwa watukufu wa darja. Hivi ndivyo alivyopanga mwenyezi mungu na wala si utashi wakiumbe yeyote bali majaliwa yake allah. Sheikh salim amelelewa ndani ya bahari ya twarika. Sheikh salim kazaliwa ndani ya twarika na anaishi ndani ya twarika. Kwa ajili hiyo basi hapana shaka yeyete juu ya malezi yake.
Sheikh salima liondoka katika mji aliyozaliwa kwa amri ya kheir toka kwa allah juu ya sharif swaleh akakaa zawiyani na akuondoka mahala hapo ila kwa amri ya kheri toka kwa allah juu ya sheikh swaleh kumtaka sheikh salim fafungue darsa darsa l;a kusomesha elim ya dini kwa muongozo wa kitwarika. Ndipo sheikh salim alip[o fungua darsa na kusomesha. Kwa vile kalelewa katika mazingira ya kheiri na kweli na yeye kachaguliwa na mwenyezi mungu katika kuyahifadhi mafundisho mema , basi hakufanya jambo ila katika kuyahifadhi mafundisho mema basi hakufanya jambo ila mpaka apte ruksa maalum toka kwa mabwana wakubwa. Sasa namna avyopata habari allah anajua.















Sura ya Sita
Kuhamia Arusha Sheikh Saalim
 



Haukupita muda baada ya kifo cha sharifu muhdhari akaja mcha mungu mmoja mwenye asili ya kisomali akiitwa Sheikh Sufi Kabole ameendewa na sharifu swaleh amemuagiza Sheikh Sufi Kabole amchukue kutoka moshi ampeleke arusha na awe na yeye na amjengee sheikh salim zawiya yake mtaa wa Ngarenaro Arusha.
Sheikh Salim alipoambiwa amri hii toka kwa sheikh wake sharifu swaleh hakuwa na budi ila aliomba dua kwa mwenyezi mungu ili aimarishe madrasa aliyokuwa ameifungua moshi; madrasat izzadini awaswadifishe vifuani mwao muri wote wa sharifu swalehe hapo moshi na wadumu ndani ya twarika zaidi na zaidi kisha akwaaga waislam muridi wa moshi pamoja na wanafunzi wake akaondoka kwenda arusha akiambatana na sheikh sufi kabole kama alivyoagizwa na sharifu swaleh kupitia kwa huyo Sheikh Kabole. Sheikh Salim alipofika arusha akawa amemuegama akawa amemuegama sheikh sufi kabole, naye sheikh sufi kabole akatimiza yote aliyoagizwa na Sharif Swaaleh juu ya Sheikh Salim.
 Kisha akamuomba ruksa arejee zake mombasa kwani yote aliyoamriwa na allah juu ya Sharifu Swaleh kumtekelezea sheikh salim ametimiza hivyo anarudi mombasa. Sheikh salim kama ilivyokuwa wachamungu japo wapende vipi hawazuilii haki ya yeyote mbele ya allah, hivyo akamruhusu sheikh sufi kabole aende zake mombasa naye abaki arusha akiendeleza twarika.
Sheikh sufi kabole alipofika mombasa naye hakukaa muda akafariki dunia. Kufariki kwa sheikh sufi kabole kuliamsha ari na bidii kubwa ndani ya nafsi ya sheikh salim akaongeza jitihada kutimiza kile alichotarajiwa kukifanya ndani ya uislam na twarika kwa ujumla
Bila kukawia akaanza kufundisha madrasa msikiti wa mondeni na majlisul ulaa kwa mama betii, vilevile akawa akifanya kila jitihada katika kuleza twarika hadi pakajengeka ilipo zawia kuu hivi sasa matejoo-ngarenaro-arusha mjini.
Sheikh salim kafanya hayo akitarajia rehma za mwenyezi mungu na baraka za Assayyid Sheikh Abdul Qaadir na radhi za mabwana wa kubwa waliomlea na kumtukuza kimwili na kiroho . Katika kipindi hicho chote mpaka mimi kuchukua jukumu la kuyaandika haya sheikh salim hakuacha kuwa ni mwenye kuizuru madrasa aliyoicha mjini moshi chini ya mwanafuzi wake Sheikh Ramadhani Bin Khamis Ally.
Hadi leo madrasa ya izzadini imeweza kueneza matawi sehemu yote ya Tanzania bara na visiwani ikiwa na idadi ya matawi zaidi ya thelathini na tano yaliyo hai. Madrasa ya izaadini imetoa wanazuoni wengi kupitia athari ya elimu aliyoicha sheikh salim kwa baraka za masheikh na walezi wake wa kiroho.










Sura ya Saba
Kueneza Dini na Twariqa
 





Katika maisha ya sheikh Saalim alitumia muda wake mwingi kueneza na kuwafunza watu dini na twariqa. Hii ilikuwa sunna ya mtukufu wa darja mtume Muhammad na ndio mafunzo na amri aliyopewa na sheikh wake Sharif Swaaleh(Q.A.S).
Hivyo Sheikh Saalim alijikita katika kueneza dini na twariqa kwa harakati mbalimbali. Miongoni mwa harakati hizo ni pamoja na ujenzi na ufunguzi wa miskiti, madrasa, vyuo vya dini na zawia mbalimbali. Sheikh salim kupitia Twariiqatul Qaadiriyyah Arraaziqiyyah ameweza kufungua mazawia na majaalis za kidini katika mikoa takriban yote ya Tanzania.
Madrasa na misikkiti ndio idadi yake haisemekani kwani mbali na madrasa nyingine madrasa yake ya kwanza (Izzadin) ina takriban matawi yasiyo pungua thelathini na tano nchi nzima.
Kwa juhudi zake binafsi na kwa msaada wa   makhalifa wake ambao ndio washauri wake wakuu, sheikh salim aliweza kuisajili taasisi ya Twariiqatul Qaadiriyyah Arraaziqiyyah Al-jailaaniyyah kwa serikali ya Tanzania kama taasisi ya dini nchini.
Sheikh Saalim katika harakati zake ameweza kusilimisha mamia kwa maelfu ya watu hasa katika mikoa ya Singida, Tabora, Manyara, Arusha, Kilimanjaro na Dar es salaam.Sheikh Salim hakuwa msilimishaji tu bali alihakikisha alio wasilimisha wanapata elimu ya muongozo wa kiislam.
Mbali na yote hayo Sheikh Salim aliyejaa hikma, elimu, maarifa na karama ni muandishi na  mtunzi mzuri na hodari wa vitabu vya dini ya uislamu. Yote hii ni kwa ajili ya kuwagawia watu elimu mbali na njia yake ya asili aliyorithi kwa masheikh zake ya kudarsisha. Moja ya vitabu maarufu alivyotunga ni ALGHAUTHUL AADHWAM alichosimulia ndani yake maisha ya Sheikh Abdul qaadir Jailaaniy (Q.A.S)
Kwa uchache hii ndio khabari ihusuyo maisha ya bwana mkubwa wetu Swahibu Sujjadah.
والله أعلم والموافق في طريق المستقيم
Ust Musa Abdul Rahman Msele














Comments

Popular posts from this blog

القراءات العشر المتواتر(علم التجويد)

علم المعان